Wednesday, May 17, 2023

Samaki mchuzi kwa mapishi tofauti

ad300
Advertisement

Mapishi haya yanaweza kupika samaki aina yeyote – mbichi, aliyekaushwa au aliyekaangwa. Ni maalumu kwa kubadilisha ladha ya mapishi kutokana na chaguo la samaki wako. Unaweza kupata njia tofauti za kuongeza ujuzi wa kuandaa samaki wako.



Mahitaji

  • Samaki 2 (Tunatumia samaki wabichi)
  • Vitunguu maji
  • Vitunguu saumu
  • Nyanya
  • Mafuta
  • Ndimu
  • Chumvi
  • Carrots
  • Tangawizi
  • Pilipili hoho

Maelekezo

  • Andaa vitunguu saumu, tangawizi na ndimu. Tenga kitunguu saumu kwenye sehemu mbili.
  • Osha na kisha marinate samaki wako – weka tangawizi, vitunguu saumu, ndimu na chumvi.
  • Acha samaki akae kiasi – ikiwezekana kwenye jokofu – ili viungo viingie vizuri.
  • Menya vitunguu, nyanya, pilipili hoho na karoti na kisha kata vipande vidogo.
  • Weka mafuta kwenye kikaangio kilicho jikoni. Subiria yapate moto vizuri.
  • Weka samaki na ukaange hadi aive vizuri. Ukimaliza weka samaki pembeni.
  • Bandika sufuria, weka mafuta uliyokaangia samaki. Subiria yapate moto vizuri kisha weka vitunguu na uvikaange mpaka viwe vya kahawia.
  • Weka pilipili hoho na koroga mchanganyiko.
  • Weka vitunguu saumu huku ukiendelea kukoroga kuzuia visigande kwenye sufuria.
  • Weka karoti na endela kukoroga
  • Weka nyanya kisha funika kwa muda wa dakika 5. Hakikisha kuwa moto si mkali sana, bali uwe wa wastani.
  • Kamulia ndimu kwenye mchanganyiko na weka chumvi kisha koroga kiasi.
  • Weka samaki na ongeza maji kiasi (usifanye hapo kwa mama ntilie mchuzi maji tu, hapo nyumbani jaribu kuandaa mchuzi mzito)
  • Acha mboga ichemeke. Maji yakikaukia mchuzi wako utakua tayari na unaweza kula na chakula chochote.
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 comments: