Monday, September 9, 2019

FAIDA ZA MAJI YA MCHELE KWENYE NYWELE

ad300
Advertisement
Maji ya mchele yana faida nyingi kwenye ngozi na nywele.
🍃Yanalainisha  na kung’arisha nywele zako.
🍃Yanajaza nywele kwa sababu ya Amino acid inayopatikana kwenye maji ya mchele.
🍃Yanaimarisha nywele na kufungua vitundu vya ngozi (hair pores ) ili ziweze kukua vizuri.
🍃Kuondoa  miwasho na mba kichwani
🍃Kujaza nywele


JINSI YA KUANDAA
✨Andaa mchele wako robo kilo (1/4 kg - mchele aina yoyote)
✨Osha vizuri kisha weka kwenye sufuria yako safi.
✨Ongeza maji mengi au kadiria zaidi ya hapo  mchele ulipoishia maana unafyonza maji sana.
✨Weka jikoni na ufunike.
✨Acha uchemke kwa dakika 10  hivi kwa moto wa wastani (usiive) au hadi uone mchele unaanza kulainika kwa mbali.
✨Epua na uache upoe kidogo kisha chuja na kitambaa au chujio safi.
✨Weka kwenye kopo maji uliyoyachuja na ufunike vizuri usiku mzima, asubuhi ongeza maji kikombe kimoja ili kupunguza nguvu.

NB: Unaweza kutengeneza zaidi ukahifadhi kwenye friji kwa wiki mbili.

NAMNA YA KUTUMIA
✨Fanya pree poo kama kawaida ya Alovera au hot oil treatment (Ntaelekeza kwenye post inayofata)
✨Shampoo nywele zako (Paka shampoo kwenye ngozi ya kichwa, lowanisha na sugua vizuri ngozi pamoja na nywele zako)
✨Suuza na maji ya mchele na ufunike kichwa kwa dakika 30.(utasuuza na maji ya kawaida baada ya hizo dakika)
✨Fanya deep conditioning kwa dakika 30 (yoyote uliyo nayo)
✨Suuza tena nywele zako na maji ya kawaida
✨Kisha pakaa leave in conditioner yako, mafuta yako uyapendayo kwenye nywele (tumia mafuta ya maji) kwa sababu mafuta ya mgando yanaleta mba na kumalizia na cream (shea butter)
✨Style nywele zako ulivyozoea au nenda kasuke

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

1 comment:

  1. je ni nywele zikiwa zimesukwa ndo unapaka maji ya mchele

    ReplyDelete